Ujumbe wa Ufunuo – sura ya 2. 

 

 

Ujumbe kwa Efeso

Ujumbe kwa Smirna

Ujumbe kwa Pergamo

Ujumbe kwa Thiatira

 

Katika sura mbili zifuatazo kuna ujumbe kwa makanisa saba. Ujumbe huo inatuhu­su sisi pia. Tungeweza kuchunguza kila kanisa na ujumbe wake na kutafuta mafu­ndisho kwa ajili ya wakati wetu na makanisa yetu. Tungepata mafundisho mazuri na maonyo makali. Kukaripia na shukrani.

Lakini uchunguzi huo ungechukua muda mrefu, hata sasa hatutachunguza ujumbe kwa ma­kanisa saba kwa upande huo bali tunachunguza kwa upande wa unabii yaani kwa mpangilio wa muda. Kwa njia nyingine kila kanisa inawakilisha muda wake kikristo tangu wakati wa mitume hadi mwisho wa kipindi cha makanisa. Wakati wa Yohana ujumbe kwa makanisa ulikuwa ni unabii wa mambo yajayo, kwamba wokovu na ukristo na kukua vitakuwaje. Sasa tunaweza kuangalia nyuma, lakini kipi­ndi hicho waliangalia mbele. Sasa tunaweza kwanza kusoma unabii ndani ya Ufunuo na kisha tuangalie katika historia ya makanisa kama mambo hayo ni kweli kadri ya Ufunuo wa Yohana. Tukichunguza mambo kwa njia hii tutagundua ni kweli kwa kadri ya Ufunuo.      

 

EFESO (miaka 30-100)

Wakati wa makanisa kanisa la Efeso lili­kuwa kanisa la kwanza. Kanisa la Efeso ni mfano nzuri wa makanisa wakati wa mi­tume. Yale mambo yaliyokuwa Efeso yali­patikana hata ka­tika makanisa mengine ya wakati huo. Matatizo ya Efeso yaliku­wapo hata sehemu zingine na shukrani zilizopati­kana Efeso zilikuwa faida kwa makanisa mengine. Efeso inawakilisha wa­kati wa mi­tume, tangu mwaka wa thela­thini hadi mwaka wa mia moja baada ya Kristo.

1. Kwa malaika wa kanisa lililoko Efeso andika; Haya ndiyo anenayo yeye azi­shi­kaye hizo nyota saba katika mkono wake wa kuume, yeye aendaye katikati ya vile vinara saba vya dhahabu. 2. Nayajua matendo yako, na taabu yako, na subi­ra yako, na ya kuwa huwezi kuchukuliana na watu wabaya, tena umewajaribu wale wajiitao mitume, nao sio, ukawaona kuwa waongo; 3. tena ulikuwa na subi­ra na kuvumilia kwa ajili ya jina langu, wala hukuchoka. 4. Lakini nina neno juu yako, ya kwamba umeuacha upendo wako wa kwanza. 5. Basi, kumbuka ni wapi ulikoanguka; ukatubu, ukayafanye matendo ya kwanza. Lakini, usipofanya hivyo, naja kwako, nami nitakiondoa kinara chako katika mahali pake, usipotubu. 6. Lakini unalo neno hili, kwamba wayachukia matendo ya Wanikolai, ambayo na mimi nayachukia. 7. Yeye aliye na sikio, na alisi­kie neno hili ambalo Roho aya­ambia ma­kanisa. Yeye ashindaye, nitampa kula ma­tunda ya mti wa uzima, ulio katika bustani ya Mungu. (UFU 2:1-7)

Makanisa ya wakati huo yalikuwa pungufu na kupungukiwa, kama siku hizi pia. Tulisoma mstari wa kwanza kwamba Yesu alitembelea kati ya vinara, yaani kati­kati ya makani­sa. Ali­penda kukaa ndani ya makanisa yale yote saba katika Ufunuo. Kwa sababu  Yesu Kristo ni yeye yule, jana na leo na hata milele (EBR 13:8) hata leo anate­mbelea makanisani. Ni vizuri tukikaa ndani ya ma­kanisa yetu sababu Yesu anate­mbelea ma­kanisani. 

Wakati wa mitume makanisa yalikuwa na matukio mengi kazi nyingi na uvumilivu. Wakati huo uliangaliwa sana kwamba dhambi isikubaliwe maishani. Wale mitume wa uongo walijari­bu kujiingiza miongoni mwao. Lakini waliteswa na waliojifanya walitengwa kando. Wakristo waliudhiwa sana kwa ajili ya Jina la Yesu lakini ha­wa­kuchoka. Baadaye upendo wao kwa Yesu ulipoa na uamusho ukaanza kupoa. Miujiza haikuto­kea kama hapo awali. Labda haiku­tafutwa tena. Pole pole hata kazi ya Roho Mtakatifu makanisani ilipungua na kazi za watu zilio­ngezeka.

Yesu aliahidi kutoa kinara mahali pake iwapo upendo hautarejea ndani ya wachu­ngaji na wa­hubiri. Hema ya kukutania ni mfano mkubwa katika Agano la Kale. Ka­tika hema ya kukuta­nia kilikuwamo kinara pia. Kazi ya kinara na zile taa iliku­wa kumulika ile meza ya mikate iliyo­kuwa kule mbele. Mifano hiyo inamaana ya vya­kula vya rohoni ambavyo Mungu anataka kutugawia maka­nisani. Mungu anataka kwamba katika makanisa kuwe na chakula cha rohoni lakini kama upendo wa waalimu umepoa kwa Yesu, waalimu na wahubiri hawa­ioni tena ile meza ya chakula, na hawawezi ku­wagawia wakristo chakula cha rohoni. Hapo waalimu na wachungaji na wakristo watapata njaa ya kiroho. Hayo yote yanasaba­bishwa na upendo wa Yesu kupoa ndani ya wachungaji.

Historia ya makanisa inatuelewesha kwamba pole pole makanisa yalianza kujitoa, hawa­ku­tunza ile nguvu waliyokuwa nayo.  Yaani hawakutubu.

Hivyo uamsho ulianza kupungua moto ka­tika karne zilizopita na makanisa mengi yali­anza kwenda pembeni na uongozi wa Roho Mtakatifu. Kinara kilitolewa ma­hali pake, chakula cha kiroho kilipungua makanisani. Kama chemchemi ya rohoni ilienda pembeni na kukauka, Mungu alifungua zingine na uamsho wa kiroho mpya. Kila mara kuna makanisa yenye nguvu na yale yaliyokauka.

Wachunguzi wa Biblia wanafikiri kwamba shemasi mmoja wa Yerusalemu kwa jina Ni­kolao (MDO 6:5) baadaye alianguka na ku­leta mafundisho ya uzushi. Lakini hatujui, wala si muhimu kujua. Pia watu wali­fundishwa kwamba kazi za utumishi wali­pewa baadhi ya watu. Wakristo wa kawaida walikatazwa ku­fanya kazi ya Mungu na kushuhudia. Mafundisho hayo yalileta maisha ya ukahaba na uhuru wa mwili. Wa­liambiwa kwamba tume­wekwa huru kutoka utu­mwa wa dhambi, tuna­ishi tuna­vyotaka, dhambi haitatuangamiza. Walisema: Upata­nisho unatosha. Hivyo mwili ulipewa uhuru wa kuishi unavyotaka katika uchafu.

Ni kawaida kwamba wengi walipoteza imani yao kwa sababu ya mafundisho ya aina hiyo.

Mawazo ya aina hii na uhuru wa mwili ulichukiwa mwanzoni huko Efeso, na hata Yesu alichukia, kama tulivyosoma. Yesu alikataa ukuhani to­fauti bali wote ni wa­tendakazi wake siyo ma­kuhani peke yake. Hivyo kila mmoja ana wa­jibu wa kuta­ngaza Injili na siyo wa­tumishi tu. Baada ya mafu­ndisho ya Wanikolai kuenea, wali­tokea mababa wa kanisa na majengo ya Wakatoliki.

Kutokea kwa kanisa la Katoliki kulisaba­bisha kanisa la Efeso kwenda pembeni. Yesu ana­elekeza somo hili kwa mtu mmoja mmoja akisema, kwamba: Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. (UFU 2:7a) Yeye ashindaye, ni­tampa kula matunda ya mti wa uzima, ulio katika bustani ya Mungu. (UFU 2:7b)

Ushindi haupatikani bila mapambano. Yeye atakayepambana na kushinda, kuna ahadi nzuri kwa ajili yake. Yeye asiangalie wakristo wengine bali apambane mbele za Mungu wake. Hata wengine wakianguka, wewe usianguke. Usiwaige wengine kama siyo wa­zuri.

Efeso inatupa mfano wa wakati wa kiroho, ambayo ilikuwa wakati wa Yohana. Mwaka wa thelathini hadi mia moja baada ya Kristo.

 

SMIRNA (miaka 100-313)

Baada ya kanisa la Efeso barua ilikuja kwa kanisa la Smirna.  Kanisa la Smirna li­na­wakilisha wakati na maisha ya kiroho kua­nzia mwaka wa mia moja baada ya Kristo na kuendelea kama miaka mia mbili mbele, ku­tukaribia sisi. Kwa usahihi hadi mwaka wa mia tatu kumi na tatu baada ya Kristo. 

Smirna ni sawa na Mirha, yaani manemane. Manemane ni mfano wa mateso. Kani­sa la Smirna ni la wa­kati wa ma­teso, ilipata dhiki nyingi kwa ajili ya imani yake. 

8. Na kwa malaika wa kanisa lililoko Smirna andika; Haya ndiyo aneneyo yeye aliye wa kwanza na wa mwisho, aliyekuwa amekufa, kisha akawa hai. 9. Naijua dhiki yako na umaskini wako, (lakini u tajiri) najua na matukano ya hao wase­mao ya kuwa ni Wayahudi, nao sio, bali ni sinagogi la Shetani. 10. Usiogope mambo yatakayo­kupata; tazama, huyo Ibilisi atawatupa baadhi yenu gerezani ili mjaribiwe, nanyi mtakuwa na dhiki siku kumi. Uwe mwami­nifu hata kufa, nami nitakupa taji ya uzima. 11. Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye hatapatikana na madhara ya mauti ya pili.  (UFU 2:8-11)

Karne ya kwanza sehemu nyingi Wayahudi na Wanasariti, yaani wafuasi wa Yesu, wali­kuta­nika ndani ya sinagogi moja.  Mara nyingine Wayahudi waliwapinga wa­fuasi wa Yesu na mara zingine waliwakubali. Baa­daye Wayahudi sehemu zote wa­lianza kuwapinga na kuwachukia wafuasi wa Yesu. Hata ma­kaisari wa Rumi wa­liwapi­nga na kuwatesa.

Tulisoma, kwamba kanisa liliambiwa kwamba nanyi mtakuwa na dhiki siku kumi. (UFU 2:10b)  Tunge­weza kusoma katika historia kwamba kua­nzia mwaka wa si­tini na tatu hadi mwaka wa mia tatu kumi na mbili tunaona kwamba muda wa dhiki uligawanywa vipindi kumi yaani "siku kumi"!

Kanisa halikukemewa tu bali watu walitiwa moyo pia. Matezo yalimalizika baada ya kaisari Konstantino kukiri dini ya kikristo kuwa dini ya kiserikali. Mateso yali­isha na wakati huo wakristo wali­fikiri kwamba utawala wa Mungu wa miaka elfu moja umefika, saba­bu hawateswi tena. La hasha, wakati wake ulikuwa bado.

Smirna inawaelezea wafia Kristo waliope­leka kanisa mbele. Kanisa linawakilisha muda baada ya Efeso yaani mwaka wa mia moja hadi mwaka wa mia tatu kumi na tatu baada ya Kristo.

 

PERGAMO (miaka 313-500)

12. Na kwa malaika wa kanisa lililoko Pergamo andika; Haya ndiyo Anenayo yeye aliye na huo upanga mkali, wenye makali kuwili. 13. Napajua ukaapo, ndipo penye kiti cha enzi cha Shetani; nawe walishika sana jina langu, wala hukuikana imani yangu, hata katika siku za Antipa shahidi wangu, mwaminifu wangu, aliye­uawa kati yenu, hapo akaapo Shetani. 14. Lakini ninayo maneno machache juu yako, kwa kuwa unao huko watu washikao mafundi­sho ya Balaamu, yeye aliye­mfundisha Balaki atie ukwazo mbele ya Waisraeli, kwamba wavile vitu vilivyoto­lewa sadaka kwa sa­namu, na kuzini. 15. Vivyo hivyo wewe nawe unao watu waya­shikao mafundisho ya Wanikolai vile vile. 16. Basi tubu; na usipo­tubu, naja kwako upesi, nami nita­fanya vita juu yao kwa huo upanga wa kinywa changu. 17. Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye nitampa baadhi ya ile mana iliyofichwa, nami nitampa jiwe jeupe, na juu ya jiwe hilo limeandikwa jina jipya asilolijua mtu ila yeye anayelipokea. (UFU 2:12-17)

Huko tunapata kanisa jingine linalofuata mw­aka wa mia tatu kumi na tatu hadi mia tano baada ya Kristo. Kanisa la tatu ni Pergamo. Maana ya jina la Pergamo ni: Maisha ya ndoa. Siyo ndoa halali yaani aina ile tunaoelezwa kwenye Biblia, bali isiyo halali.  Yaani kuishi kama ndoa halali, lakini kihalali siyo ndoa. Ndoa ambayo hajafungwa kihalali. Biblia inaita maisha haya ni uasherati. Huo siyo mpango wa Mungu, kama ndoa.

Wakati wa Pergamo ulikuja baada ya wakati wa Smirna. Wakati wa Pergamo ulie­ndelea kama miaka mia mbili hivi mpaka mwaka wa mia tano.

Mateso yaliisha baada ya dini ya kikristo kuanzishwa kama dini ya kiserikali. Kati­ka mataifa mengi serikali inatetea dini fulani na wakuu wa serikali wanaamua mambo ya makanisa pia. Wale vio­ngozi si lazima wawe na wokovu. Wanaweza kuwa wenye dhihaka.

Mateso yaliisha na Wakristo wa Pergamo walifurahi na ku­sema: "Sasa utawala wa Mungu wa miaka elfu ume­anza. Furaha yao haikudumu muda mrefu kwani kilicho gunduliwa kilikuwa "ndoa isiyohalali". Historia inaeleza wapagani walianza kuingia makanisani. Wao walikuwa wengi na kwa sababu mambo yalifa­nyika kwa kupiga kura, wao waliokuwa wengi walishinda.

Pole pole wale wasiookoka walianza kuwa­tesa wale wakristo waliokuwa kanisani.

Katika mstari wa kumi na tatu unatuambia kwamba ukaapo, ndipo penye kiti cha enzi cha Shetani. Wapergamo wasiookoka wali­abudu sana miungu mingine. Ma­dhabahu ya sanamu Zeu ya ilikuwapo huko na hekalu la Asklepios.  Zeu alikuwa sanamu aliyeabu­diwa kama mungu wa mbingu na mwanga. Pia alikuwa mungu wa sanamu kwa wale wote. Watu waliamini hivi. Asklepios aliku­wa akasimamia mati­babu. Ishara yake ilikuwa nyoka aliye hai.

Mji huu mdogo uliongozwa kwa ibada za sanamu yenye nguvu.  Kwa sababu watu waliobu­du sana sanamu hiyo ilimaanisha adha na mateso kwa wakristo. Walio wa Yesu walipata shida, lakini hawakumkana.

Tulisoma kuhusu mtu moja Antipa. Historia ya kikatoliki inatueleza kwamba Anti­pa ali­batizwa akiwa na miaka kumi na tatu, alikufa akite­tea wokovu akiwa na mia­ka ti­sini na tisa.

Mafundisho ya Balaamu yaliingia kanisani. (Mstari 14)  Yaani mtu anaweza kuwa wa dini fula­ni, in­gawa hana toba ya kweli. Hii siyo sahihi, hii ilikuwa uhuru wa mwili. Kanisa lilikubali uasherati na mialiko yake. Pia mafu­ndisho ya Wanikolai yalikubaliwa, hayo yalichukiwa huko Efeso. Watu waliishi kwa njia ya ukahaba na walitegemea kwamba neema yatosha. Yesu alichukia na kukataa mambo haya. Hata wachungaji walikuja juu ya wakristo. Zamani wachungaji waliwahu­dumia wakristo lakini sasa walitawala.

Tusome Petro wa kwanza sura ya tano, mi­stari ya pili na tatu.

2. lichugeni kundi la Mungu lililo kwenu, na kulisimamia, si kwa kulazimishwa, bali kwa hiari kama Mungu atakavyo; si kwa kutaka fedha ya aibu, bali kwa moyo. 3. Wala si kama wajifanyao mabwana juu ya mitaa yao, bali kwa kujifanya vielelezo kwa lile kundi.

Siyo kama wajifanyao mabwana,... bali kwa kujifanya vielelezo kwa lile kundi. Hata sisi tu­nasumbuliwa na mafundisho ya Wanikolai. Sisi tena siyo watumishi wa kanisa na wakristo bali tunataka kuwatawala. Wachungaji wanahudumia kanisa kwa ku­wagawia mazuri, maarifa ya rohoni na cha­kula cha rohoni. Mafundisho ya Wanikolai yalileta utawala mbaya kanisani ambayo Yesu aliyachukia na anachukia siku hizi pia. Wapergamo walike­mewa kwa kukubali mambo hayo.

Kanisa lilikuwa hivyo wakati wa Pergamo. Yaani wakati wa mia tatu hadi mia tano. Kanisa Katoliki lilianza hivi taratibu.

 

THIATIRA (miaka 500-1500)

Kanisa la nne ni la Thiatira. Hii ilikuwa baada ya wakati wa Pergamo. Muda wa Thiatira ulichukuwa miaka elfu moja. Muda wa Thiatira ulichukua wakati wa kanisa la kato­liki. Kuanzia mwaka wa mia tano mpaka wakati wa Lutheri kama miaka elfu na mia tano.

18. Na kwa malaika wa kanisa lililoko Thiatira andika; Haya ndiyo anenayo Mwana wa Mungu, yeye aliye na macho yake kama mwali wa moto, na miguu yake mfano wa shaba iliyosuguliwa sana. 19. Nayajua matendo yako na upendo na imani na huduma na subira yako; tena kwamba matendo yako ya mwisho yamezidi yale ya kwanza. 20. Lakini nina neno juu yako, ya kwamba wamridhia yule mwanamke Yeze­beli, yeye ajiitaye nabii na kuwafundisha watumishi wangu na kuwapoteza, ili wazini na kula vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu. 21. Nami nimempa muda ili atubu, wala hataki kuutubia uzinzi wake. 22. Ta­zama, nitamtupa juu ya kitanda, na hao wazinio pamoja naye, wapate dhiki kubwa wasipotubia matendo yake; 23. nami nita­waua watoto wake kwa mauti. Na ma­kanisa yote watajua ya kuwa mimi ndiye achungu­zaye viuno na mioyo. Nami nitampa kila mmoja wenu kwa kadiri ya matendo yake. 24. Lakini nawaambia ninyi wengine mlioko Thiatira, wo wote wasio na mafun­disho hayo, wasiozijua fumbo za Shetani. kama vile wasemavyo, sitaweka juu yenu mzigo mwingine. 25. Ila mlicho nacho kishikeni sana, hata nitakapokuja. 26. Na yeye ashindaye, na kuyatunza matendo yangu hata mwisho, nitampa mamalaka juu ya mataifa, 27. naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, kama vyombo vya mfiny­anzi vipo­ndwa­vyo, kama mimi nami nilivy­opokea kwa Baba yangu. 28. Nami nitampa ile nyota ya asubuhi. 29. Yeye aliye na si­kio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. (UFU 2:18-29)

Baadhi ya wakristo wa Thiatira walipata sifa na wengine walikemewa. Historia inaeleza kwamba uamusho ulitokea sehemu mbali mbali na makanisa mengine yali­zaliwa. Ma­kanisa ya macahche yalipotea zaidi na mafu­ndisho ya Biblia na hata Roho Mtakatifu. Makanisa hayo yalikufa kiroho. Ndiyo maana baada hayo baadhi wali­pata shukrani na wengine kukemewa. Uamsho ulileta watu kwa Yesu na uliongoza watu kwenda mbinguni na uamsho ulishukuriwa. Yale ma­kanisa yaliyokufa yali­yo­potosha watu upo­tevuni yalikemewa.

Thiatira alikuwa na mpotoshaji, jina lake ni Yezebeli. Yeye alikuwa mwanamke aliyejiita nabii. Wengi walimfuata yeye na walianga­mia pia. Yezebeli ni mfano wa dini ya kika­toliki aliyeleta kule kanisani kuabudu Maria. Kanisa Katoliki linawafundisha watu kwa mafundisho ya Maria.

Thiatira walikuwepo wakristo wengi wale waliopewa ahadi nzuri za ushindi. Ukatoliki uli­kuwa mkubwa na ulikuwa ni kanisa lililopotoka. Watu wengi walipo­tea pia. La­kini watu wachache ha­wakupotea. Tena Mungu alikuwa pamoja na wale waliotaka ku­mfuata. Historia inaeleza kwamba uamusho ulitokea sehemu mbali mbali.

Mambo ya kanisa la Thiatira yalikuwa na unabii wa kuzaliwa kwa katoliki. Ufunuo huo uli­kuwa kamili.

Turudie kwa ufupi.

Kanisa la Efeso linawakilisha historia ya wakati wa mitume yaani mpaka mwaka wa mia moja baada ya Kristo. Smirna tokea mwaka mia moja hadi mia tatu kumi na tatu. La tatu ni Pergamo, inawakilisha miaka ya mia tatu kumi na tatu hadi mia tano. Ya nne ni Thiatira. Matukio yake yalibashiri dunia ya ukiristo itakuaje mia­ka ya mia tano hadi elfu moja mia tano. Sasa tunaona kwamba Ufunuo ulitimia kimaandi­ko.

 

---------------------------------------------------------------------------------------------------------