Teuvo Kopra:

 

 

            ZABURI YA WACHUNGAJI

 

 

 

 

              

 

  

                         Zaburi 23

 

 

 

1. Bwana ndiye mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu. 2. Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, kando ya maji ya utulivu huniongoza. 3. Hunihuisha nafsi yangu; na kunio­ngoza katika njia za haki kwa ajili ya jina lake. 4. Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, sitaogopa ma­baya; kwa maana wewe upo pamoja nami, gongo lako na fimbo yako vyanifariji. 5. Waandaa meza mbele yangu, ma­choni pa watesi wangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, na kikombe changu kinafurika. 6. Hakika wema na fadhili zitanifuata siku zote za maisha yangu; nami nitakaa nyu­mbani mwa Bwana milele. (ZAB 23:1-6)

 

Tusome pia Petro wa kwanza sura ya tano na mstari wa kwanza hadi wa nne.

 

1. Nawasihi wazee walio kwenu, mimi niliye mzee, mwenzi wao, na shahidi wa mateso ya Kristo, na mshirika wa utukufu utakaofunuliwa baadaye; 2. lichugeni kundi la Mungu lililo kwenu, na kulisimamia, si kwa kulazimishwa, bali kwa hiari kama Mungu atakavyo; si kwa kutaka fedha ya aibu, bali kwa moyo. 3. Wala si kama wajifanyao mabwana juu ya mitaa yao, bali kwa kujifanya vielelezo kwa lile kundi. 4. Na Mchu­ngaji mkuu atakapodhihirishwa, mtaipokea taji ya utukufu, ile isiyokauka. (1PET 5:1-4)

 

Hapa tunaelezwa juu ya kazi yetu. Sisi ni wachungaji ndani ya kanisa la Mungu. Katika mstari wa nne tunae­lezwa juu ya mchungaji mkuu. Yesu ni Mchungaji Mkuu nasi ni wasaidizi wake. Sisi ni wachungaji wa mshahara. Mshahara unatusubiri tukifika mbinguni. Kama tunatumikia kanisa vizuri tutapata mshahara mkubwa zaidi, lakini tukitumikia vibaya tunaweza ku­baki bila ya mshahara.

 

Mchungaji Mkuu na wasaidizi wake wana kazi yao. Ni ujuzi wa Mungu kulinganisha kanisa na kundi la kondoo. Wakristo kanisani wanali­nganishwa na kondoo. Ndani ya kundi la kondoo kuna mengi yanayofanana hata kanisani. Ndio maana kundi la kondoo ni mfano mzuri wa kanisa. Pia kondoo wana ta­bia sawa sawa zinazofanana na Wakristo. Ndio maana kondoo ni mfano mzuri wa washirika wa kanisa.

 

Ko­ndoo wanataka wawe pamoja kama Wakristo kanisani. Kondoo wanamfuata mchungaji kama Wakristo ndani ya kanisa. Yesu anatangulia nasi tunamfuata. Na pia Wakristo wanawafuata wachungaji wa kanisa. Ndio maana ni muhimu sana kuangalia jinsi sisi wachungaji tunavyoishi na kuenenda. Tunapochunga kanisa la Mu­ngu ni vizuri kukumbuka kwamba mwenye kundi ni Yesu mwenyewe. Sisi ni wasaidizi. Kundi siyo letu. Kanisa siyo letu. Kanisa ni la Mchungaji Mkuu, yaani la Yesu Kristo. Sisi tunachunga kondoo lakini kondoo siyo mali yetu. Ni muhimu sana kukumbuka hayo.

 

Kuna kondoo mbali mbali ndani ya kundi. Na pia ndani ya kanisa kuna Wakristo tofauti tofauti. Nasi tu­napaswa kuwachunga wote. Hatuwezi kuwabadilisha wote wafanane. Mchungaji Mkuu ametuumba tofauti tofauti. Anataka tukubali kwamba sisi watu ni tofauti tofauti. Mchungaji Mkuu anakubali hayo nasi tuna­paswa tuyakubali pia. Ndani ya kondoo wa duniani kuna wengine wanono. Wanakula chakula kingi. Hata kanisani kuna watu wanene sana kiroho. Yaani wana­kula chakula kizuri cha kiroho ndio maana ni wanene.

 

Pia kondoo wa duniani kuna kondoo wengine walioko­nda. Labda ni wagonjwa au hawali wakashiba. Kanisani kuna wengine ambao wamekonda kiroho. Inawezekana hawaendi kanisani mara kwa mara. Au hawasomi Biblia na hivi hawapati chakula cha kiroho. Kwa maana hiyo wamekonda kiroho. Labda wengine kanisani ni wago­njwa kiroho. Ndani ya kundi la kondoo kuna kondoo wengine wenye mimba. Ndio maana mchungaji anawa­tembeza taratibu ili baadaye kondoo waweze kuzaa watoto wenye afya.

 

Mara kwa mara mchungaji anachu­nguza kundi la kuchunga ili hali ya kondoo ingekuwa nzuri. Yeye hawapeleki haraka wala pole pole sana. Ni sawa hata ndani ya kanisa. Ni lazima tuchunguze Wa­kristo kanisani. Na kuwaongoza kwa njia inayofaa, ili Wakristo wajisikie vizuri.

 

Iwapo Wakristo wanaendelea vizuri wanaweza kuendelea kuzaa kondoo wengine wapya. Hali ya kiroho ikiwa nzuri kanisani inakuwa vizuri zaidi. Wakipata chakula kizuri cha kiroho wana afya nzuri kiroho pia. Ni muhimu kutoa chakula kizuri cha kiroho na chenye afya njema.

 

Pia kuna kondoo we­ngine ndani ya kundi  wanao gonga wenzao. Na wana­sababisha matatizo mara kwa mara kwa mchungaji. Pia kanisani kuna wale wanao pigana na kugombana na wenzao. Hao wanaleta matatizo kwa wachungaji kani­sani lakini tukumbuke kwamba hao pia ni wapenzi wa Mchungaji Mkuu, yaani Yesu Kristo. Tuwapende na hao pia ingawa si kazi rahisi.

 

Ndani ya kundi la kondoo kuna wengine wagonjwa. Wengine hawatembei vizuri, wanatembea kwa kuchechemea. Ndani ya kanisa kuna pia wengine ambao hawajakuwa vizuri kiafya. Wengine wanaendelea kuchechemea. Wengine wanaanguka zaidi ya wengine. Mara nyingine inatulazimu kuwabeba we­ngine. Hawa wanatuletea matatizo. Tunahuzunika na mienendo yao.

 

Ni lazima tukumbuke kwamba kanisa siyo letu. Wakristo sio wetu bali wa Yesu. Lazima tue­nende nao kama vile Yesu Kristo anavyoenenda na sisi. Yeye ni Mchungaji Mkuu sisi ni wasaidizi wake. Tuna­paswa kuuliza matakwa yake ili tuweze kuvumiliana na hao Wakristo wenye matatizo.

 

Ndani ya kundi la ko­ndoo kuna wengine wazee na wengine vijana. Ndivyo ilivyo ndani ya kanisa. Kondoo wanatofautiana katika tabia. Wengine wana upungufu katika tabia. Ndivyo ilivyo hata kanisani. Mara nyingine tunaweza kusha­ngaa kwa nini Wakristo wanaenenda hivyo. Au tuna­shangaa kwa nini wanaongea hivyo. Wanatofautiana. Mungu ametuumba tofauti tofauti. Tusijaribu kuwaba­dilisha wafanane kwani Mungu amewaumba kwa hali hiyo.

 

Mchungaji wa kondoo ana kazi kidogo sana pa­moja na kondoo wanaotii na wazuri. Lakini wale wenye matatizo wanaleta na wanasababisha matatizo mengi kwa wachungaji. Ndani ya kanisa wengine wanawasa­babishia wachungaji matatizo mengi na wengine mata­tizo madogo madogo tu. Muda mwingi mchungaji ana­wahudumia wale kondoo wenye matatizo. Ni sawa hata kanisani wachungaji muda mwingi wanajaribu kuwa­saidia wale ambao wana matatizo na wanaogombana na Wakristo wengine na watu wengine.

 

Ndio maana wa­chungaji wanapata ndani yao picha isiyo sahihi na ya kukanusha kundi kwa maana wanafanya kazi kati ya matatizo mengi. Ndio maana sisi wachungaji tunahitaji maombi mengi na kusoma Biblia kwa bidii ili tuone kanisa kwa macho ya Mungu. Tukiangalia kanisa na Wakristo kwa macho ya mwilini tunaona tofauti na kama vile tungewaangalia kwa macho ya Mchungaji Mkuu Yesu Kristo.

 

Akiwepo mgonjwa katika kondoo wakufugwa mchu­ngaji anamchinja. Hivyo anapata kundi la hali ya juu. Hapo wanao kondoo wazuri na wenye afya tu. Sisi tu­kiwa wachungaji katika kundi la kondoo wa Yesu kani­sani, tunapaswa kufanya yale anayotaka Mchungaji Mkuu. Mchungaji Mkuu wetu hajaturuhusu kuchinja hata kama kuna mgonjwa au mwenye hitilafu na aliye konda. Haturuhusiwi kuchinja hata yule anayowapa kondoo wenzake matatizo mara kwa mara, Wakristo wengine kanisani. Hata wale wanaotupiga na kutugonga gonga. Kuchinja ni sawa na kama kutenga Mkristo fu­lani ambaye amekwisha kuokoka. Au tunakataa atafika mkutanoni. Au tunakataa ushirikiano na Wakristo we­ngine.

 

Lakini fulani akipoteza hali yake ya kiroho na asitubu baadaye huyo amekufa kiroho. Huyo aliyekufa kiroho ni lazima atengwe lakini siyo yule Mkristo dhaifu kama ana uhai wa kiroho. Kondoo hawa wa kawaida akifa katika kundi anatolewa. Hata wale wanao eneza magonjwa ya kuambukiza. Ni sawa ndani ya kanisa la kiroho: walio rudi nyuma au walio kufa kiroho na ha­wataki kutubu ni lazima watengwe. Hata ambao kukaa kwao kanisani wanachafua sana kanisa. Kutenga kufa­nyike kwa njia nzuri ili hata baadaye aweze kwa urahisi kurudi kanisani.

 

Wakati wa Agano la Kale waliofanya kazi ya kiroho waliitwa makuhani. Kama fulani alifanya dhambi alie­nda hekaluni kwa kuhani. Alikuwa na kondoo kwa ajili ya dhabihu. Mwenye dhambi aliungama dhambi zake mbele ya kuhani na kondoo alichinjwa kwa ajili  ya dhambi zake. Hivyo mwenye dhambi alisamehewa. Huu ni mfano wa kazi ya dhabihu aliyofanya Yesu alipokufa msalabani kwa ajili yetu. Kuhani aliwatumikia wenye dhambi katika eneo la hekalu. Kuhani alisikiliza mau­ngamo ya dhambi na alisaidia katika kuchinja. Yaani kuhani alikuwa mchinjaji. Mtu alipofanya dhambi ku­hani alichinja kondoo. Hayo yalifanyika wakati wa Agano la Kale.

 

Katika Agano Jipya sisi siyo makuhani yaani wachinjaji bali wachungaji. Haturuhusiwi kuchi­nja kondoo kwa sababu ya dhambi Yesu alikwisha chi­njwa kwa ajili ya wenye dhambi. Bali kama kondoo fulani yaani aliyeokoka akaanguka dhambini ni kazi yetu kumsaidia ili apate msamaha. Hatumtengi bali tunajaribu kumtibu. Mchungaji wetu Mkuu hajatupa ruhusa ya kuchinja bali ametuamuru kulisha na kuchu­nga kondoo. Sisi ni wachungaji ndani ya kundi la ko­ndoo wa Yesu.

 

Ndani ya kundi la kondoo kuna kondoo tofauti. Tu­napowachunga mara nyingine tunawashangaa. Au hata tunaweza kukasirikia mmoja wao. Mara zingine tuna­shangaa sana na matendo ya wengine ndani ya kundi usemi wake wa matendo yake. Tunataka wote katika kundi letu wawe wazuri na wawe na tabia njema. Ndio maana wakati mwingine tunatumia hasira au tunatoa fimbo. Na fulani akiwa ameshindikana tunataka tumpe­leke machinjioni yaani kutenga kanisani. Ndio ni lazima tuwe na adabu kanisani lakini tunaweze kuwa wakali kupita kiasi.

 

Kutokuwa na utii ni jambo mbaya kanisani. Katikati ya matatizo hayo tunapaswa kukumbuka kwa­mba kundi siyo letu. Kondoo siyo wetu. Sisi ni wachu­ngaji wa kundi la kondoo wa mgeni. Mwenye kundi yaani Yesu anatuambia wachungaji: "Ni kundi langu. Kondoo ni kondoo wangu. Mimi nimekuwa uwe mchu­ngaji si mchinjaji." Mwenye kondoo anaendelea ku­sema: "Unisaidie kuwasafirisha kundi la kondoo hadi nyumbani." Ni kazi yetu kuwasafirisha kundi la Yesu ili siku moja wafike mbinguni.

 

Tulisoma Zaburi ya ishirini na tatu. Inaeleza juu ya mwenendo wa kondoo mmoja, yaani mwenendo na maisha ya aliyeokoka. Ujumbe wa Zaburi hii unaanza kwa maisha ya mwanzoni wa aliyeokoka na kuendelea katika maisha ya wokovu hadi mwisho.

 

Tulisoma kwa­nzia mstari wa kwanza. Bwana ndiye mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu. (ZAB 23:1) Mchungaji Mkuu anataka kuwapeleka kondoo wote yaani waliookoka katika hali hii. Lakini kwa sababu Yesu hayuko nasi kimwili anatutumia sisi. Yeye ametupa sisi wasaidizi wake kazi ya uchungaji.

 

Katika Zaburi hii anatueleza ji­nsi sisi tunavyopaswa kuchunga kondoo yaani Wakristo ndani ya kanisa. Aliyeokoka karibuni anapaswa kujua kwamba amepata hazina nzuri sana. Pia afundishwe na ajue kwamba Yesu ni mchungaji wake na siyo wazee au wahubiri. Sisi ni wasaidizi tu.

 

Anapaswa kujua kwamba amepata utajiri mkubwa katika maisha yake, amepata wokovu moyoni mwake. Ingawa atapungukiwa na vitu vingine vya duniani lakini amepata hazina kubwa na utajiri wote wa duniani ni takataka mbele yake. Yeye amesamehewa dhambi zake na anasafiri kwenda mbi­nguni.

 

Tulisoma mstari wa pili kwamba: Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, kando ya maji ya utulivu huniongoza.  (Zab 23:2) Kondoo anaweza kula chakula kizuri. Kondoo siyo mnyama wa mapambano kama simba. Kondoo siyo mnyama wa kazi kama punda au fahali. Kazi ya kondoo ni kula, kupumzika na kuzaa kondoo wengine. Ndio maana ni muhimu aliyeokoka apate chakula kizuri cha kiroho na apumzike.

 

Walio­koka wengi wana njaa ya kiroho. Tuwape chakula. Ni kazi ya mchungaji kuwapeleka kwenye malisho mazuri. Pia tulisoma  kando ya maji ya utulivu huniongoza. Biblia inatumia mifano mingi. Tumeona kwamba kanisa linafananishwa na kundi la kondoo. Mkristo anafanani­shwa na kondoo. Na pia maji ina mifano mingi. Biblia neno la Mungu ni kama maji. Baraka ni kama maji. Ujazo wa Roho Mtakatifu ni kama maji.

 

Tunapomwo­ngoza aliyeokoka kando ya maji ina maana kwamba tunamwelekeza katika kusoma neno la Mungu. Na pia kupokea baraka mbali mbali za kiroho. Ni muhimu sana ajazwe na Roho Mtakatifu. Mchungaji Mkuu ametu­weka tuwe wasaidizi wake ili malengo yake juu ya ali­yeokoka yatimia. Maji na chakula ni muhimu kwa ko­ndoo. Bila ya hayo kondoo anadhoofika na hatimaye kufa. Ni sawa kwa Wakristo chakula cha kiroho na ba­raka za rohoni ni muhimu. Bila hayo wanapoteza mai­sha yao ya kiroho na labda hawatafika siku moja mbi­nguni.

 

Watu wakiwa na njaa wanakuwa wakali na wa­nagombana hata kwa kitu kidogo. Kama kanisani kuna njaa ya kiroho wana gombana mara kwa mara. Nime­kuwa mchungaji ndani ya makanisa ambapo ugomvi umesababisha makanisa kuharibika. Nimeenda kwenye kanisa iliyobomoka na nimehubiri neno la Mungu. Ni kama mkate yenye uhai. Wao wamekula chakula cha kiroho na kupokea baraka za rohoni wao wamepata nguvu na afya. Makanisa yamepata uvuvio. Wakristo wamerudi tena kanisani.

 

Kama ningalijaribu kuwachapa ili warudi nisingalifaulu. Kanisa ambao limepata fimbo linazidi kuharibika. Bali nimewaleta pamoja kwa neno la Mungu, kwa chakula kiroho. Chakula kinawaungani­sha watu, wanakuja kwa sababu wanaweza kula chakula kizuri. Wakristo wasipopata chakula cha kiroho wanae­nda kutafuta chakula katika makanisa mengine au ma­hali pengine. Kule wanaweza kupata chakula chenye sumu inayoweza kuharibu maisha yao ya kiroho. Kazi ya mchungaji ni kuwapeleka kundi katika malisho ma­zuri waweze kula na kupumzika.

 

Pia wanywe maji ma­safi. Kondoo hajui kutafuta mwenyewe ndio maana anahitaji mchungaji. Ni sawa hata kwetu kanisani. Wa­chungaji wana kazi kubwa muhimu. Tupate wapi maji masafi? Yaani tupate wapi chemchemi za baraka kwa Wakristo ili iwe faida kwao hata milele? Ndani ya che­mchemi kuna maji. Biblia inaeleza juu ya chemchemi mbali mbali za baraka na tunataka kuwaelekeza Wakri­sto huko. Wanapo kunywa kwenye chemchemi hizo wanapata baraka.

 

Maana kwako Wewe iko chemchemi ya uzima, katika nuru yako tutaona nuru. (ZAB 36:9)

Yaani tunapowaongoza waliookoka karibu na Mungu wataweza kunywa ndani ya chemchemi za baraka. Pia wanaona nuru wanapokaa karibu na Mungu.

 

Kinywa chake mwenye haki ni chemchemi ya uzima; bali jeuri hufunika kinywa chake mtu mwovu,  (MIT 10:11)

Tunapozungumza na watu vinywa vyetu vinapaswa kuwa chemchemi ya uzima. Wakristo wanataka kuzu­ngumza na wachungaji kwa sababu wanataka kupata burudisho la kiroho.

Sheria ya mwenye akili ni chemchemi ya uzima, ili kuepu­kana na tanzi za mauti. (MIT 13:14)

Tu­napofundisha kanisani Mchungaji wetu Mkuu anataka mafundisho yetu yawe kama chemchemi ya uzima. Hiyo ikiwepo Wakristo wanapata kunywa maji masafi.

 

Kumcha Bwana ni chemchemi ya uzima, ili kuepu­kana na tanzi za mauti. (MIT 14:27)

Tunataka kuwaongoza watu katika kumheshimu na kumcha Mu­ngu. Hiyo ni baraka kwao ni kama kondoo wanapoku­nywa maji mazuri.

 

Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwake aliye nao; bali kufundishwa kwa wapumbavu ni upuzi wao. (MIT 16:22)

Wakristo wanapopata ufahamu wa wokovu zaidi hiyo ni chemchemi ya uzima kwao. Ndio maana Mungu ametu­chagua katika kazi ya uchungaji ili kupitia sisi aweze kulisha kundi lake, kanisa lake. Pole pole kondoo ana­kuwa na kupata nguvu.

 

Lakini chakula kigumu ni cha watu wazima, ambao akili zao, kwa kutumiwa, zimezoezwa kupambanua mema na ma­baya. (EBR 5:14)

Hii inatokea taratibu. Hivyo kazi yetu katikati ya Wakristo inapungua. Lakini tu kama yeye amekuwa vizuri kiroho. Ni hivyo kama tutawalisha vizuri na wa­takua baadaye tutapata kazi rahisi zaidi.

 

Lakini tukifa­nya kazi yetu vibaya Wakristo watabaki kuwa watoto siku zote. Wao hawajakuwa kiroho bali wao wanakuwa watoto wa kiroho. Tulisoma Zaburi ishirini na tatu, mstari wa tatu: Hunihuisha nafsi yangu; (Ps 23:3a) Mchungaji Mkuu anataka kuhuisha roho za Wakristo. Kabla ya wokovu roho ilikuwa imenyauka sasa inahui­shwa. Hii ni nia ya Mchungaji Mkuu, nasi tuwe hivyo.

 

... na kuniongoza katika njia za haki kwa ajili ya jina lake. 4. Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa ma­uti, sitaogopa mabaya; kwa maana wewe upo pamoja nami, gongo lako na fimbo yako vyanifariji. (Ps 23:3b, 4)

Mchungaji anataka kuwaelekeza njia sahihi. Yesu pia anataka walio wake wafuate katika nyayo zake. Njia yake mara nyingine sio rahisi kwetu. Hatuelewi ni kwa nini anaongoza maisha yetu anavyoongoza. Njia zingine zingekuwa rahisi zaidi. Mstari wa tatu inaeleza juu ya kuongozwa katika njia ya haki.

 

Mstari wa nne inaeleza juu ya bonde la mauti. Biblia zingine mpya zaidi inae­leza kwamba:  ...bonde la giza kuu. Yaani Yesu anawa­ongoza walio wake katika bonde la mauti, bonde la giza kuu. Ninaelewa hapa kwamba inatueleza juu ya mambo magumu na majaribu makubwa. Hayo yanapatikana ndani ya maisha ya kila mmoja wetu. Wakristo wengine wanaenenda ndani ya majaribu makubwa. Wana mago­njwa, umasikini na mambo mengine magumu. Pia kuna vita na kifo. Hatujui ni kwa nini tunapelekwa huko.

 

Watu wanafikiri mtu akiteseka sana ni kwa sababu yeye ni mwenye dhambi sana. Watu wanafikiri kwamba ma­tatizo na ajali kubwa zinatokana na dhambi. Watu wa­nasema: Ukipata matatizo au ajali kubwa ni kwa ajili ya dhambi. Siyo kweli. Biblia inasema wafuasi wa Yesu wana matatizo mengi. Matatizo siyo adhabu bali yana­husu maisha ya watu wote, pia Wakristo.

 

Wakristo wa­chache sasa hivi wanatembea ndani ya bonde la uvuli wa mauti. Wana magumu makubwa. Katikati ya mambo hayo Yesu anataka kuwaongoza na kusaidia. Yesu ana­hitaji wachungaji wasaidizi waweze kuwasaidia walio katika magumu mbali mbali. Kama kanisani mchungaji yuko karibu nao na anawaelewa wanakuwa na hali ra­hisi zaidi. Hawachoki katikati ya matatizo yao makubwa kama mchungaji yuko karibu nao. Ndio maana unahita­jiwa.

 

Hata sisi wachungaji tunatembea katikati ya bonde la uvuli. Hata sisi tunajaribiwa kwa matatizo mbali mbali. Bwana wetu anataka tuweze kuzoea bonde hilo la matatizo. Tukiwa tumepazoe tunaweza kuwasaidia wale ambao wako huko hivi sasa. Na kwa sababu tume­pazoe hatupotei huko. Tunaweza kuwaongoza wale Wakristo ambao wanatangatanga huko. Kwa sababu Yesu anataka tufahamu bonde la uvuli vizuri anatupe­leka huko mara kwa mara. Hata huko kuna njia ambayo tunaweza kupita.

 

Tulisoma pia: sitaogopa mabaya; kwa maana wewe upo pamoja nami, gongo lako na fimbo yako vyanifariji. (Ps 23:3b, 4)

Watu wanaogopa katika matatizo yao. Yesu anataka awe pamoja na watu wakati wa majaribu. Lakini anatutumia sisi twende na watu hawa. Hawahitaji kuogopa kwa sababu mchungaji anatembea karibu nao.

 

Gongo na fimbo hayo hayatumiki kwa kuchapa kondoo bali ni kwa ajili ya adui. Kondoo anagundua kwamba mchungaji anamtetea. Hata sisi tunatakiwa tuwatetee wale walio katika matatizo, si kuwalaumu kwamba ni kwa ajili ya mwenendo wao mbaya ndio maana wame­potea. Mara nyingi majaribu yanakuja kwa mwongozo wa Mchungaji Mkuu. Wengine wanauliza bonde la uvuli lina faida gani? Lina faida nyingi. Ndio maana Yesu anatupeleka huko. Huko tunaweza kumjua Yesu vizuri. Tunaomba zaidi. Tunakuwa wanyenyekevu. Tunawahurumia wale walio dhaifu.

 

Waandaa meza mbele yangu, machoni pa watesi wa­ngu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, na kikombe changu kinafurika. (ZAB 23:5)

Eti bonde hilo haliendelei hata milele. Siku zingine tuna majaribu, wakati mwingine ni rahisi zaidi. Mambo ya mstari huu yanafanyika baada ya bonde la mauti. Na yanayofanana na hayo tuliyapata kabla ya bonde la ma­uti.

 

Tulisoma: Waandaa meza mbele yangu. Yaani Mchungaji Mkuu anataka kulisha kondoo wake. Tena anatumia wasaidizi yaani sisi. Kabla ya bonde la giza ya mauti kondoo alilazwa kwenye majani na kula chakula kibichi. Wakati wa majaribu hawezi kula vizuri lakini baada ya majaribu ataweza tena kula chakula cha ki­roho.

 

Tulisoma: Waandaa meza mbele yangu, machoni pa watesi wangu. Tuna watesi wengi wanaotupinga. Shetani ni mtesi mkubwa. Dhambi mbali mbali zinata­tiza maisha yetu ya wokovu. Pia sisi tuna mwili wa dhambi unaotaka dhambini. Ingawa tuna maadui na watesi wengi tunaweza bado kula chakula cha kiroho.

 

Kumfuata Yesu hakuondoi majaribu. Matatizo pia ha­yaondoi majaribu. Lakini katikati ya hayo yote tuna­weza kula chakula cha kiroho. Ni lazima wachungaji wajue hayo. Ndio maana wanajifunza hayo mara ka­dhaa.

 

Pia tulisoma: Umenipaka mafuta kichwani pangu.

Agano la Kale inaeleza juu ya kupakwa mafuta. Watu walipakwa mafuta kwa ajili ya kazi fulani, mfano mfalme. Au alipakwa kwa ajili ya kazi fulani kama na­bii. Mungu anakuza Wakristo kwa ajili ya kazi fulani. Kama wachungaji tunawasaidia wakue. Hasa wale ambao wamepita katika shule ya majaribu mbali mbali ni watumishi wazuri.

 

Tulisoma pia: na kikombe changu kinafurika. (Zab 23:5b)

Mungu anataka kuwabariki wale ambao ana­weza kuwatumia. Tunawaongoza na kuwasaidia Wakri­sto kanisani ili Mungu aweze kuwatumia zaidi. Tutu­maini ili Mungu aweze kuwatumia wao zaidi ya sisi. Hatuna wivu hata kama Mungu anawatumia Wakristo zaidi yetu. Tunaogopa kwamba Wakristo wengine wa­naweza kurudi nyuma. Lakini kama wengine wamejari­biwa na wamesimama wao wana nguvu zaidi. Hatuwezi kuogopa kwa ajili ya wokovu wa kondoo huyu. Kondoo walio kuwa wanapaswa kupewa kazi kulingana na umri wao.

 

Hakika wema na fadhili zitanifuata siku zote za mai­sha yangu; nami nitakaa nyumbani mwa Bwana milele. (Zab 23:6)

Yesu anataka Wakristo waweze kuona mai­sha ya wokovu kwa njia hii. Sio tu wakati wa baraka bali kila siku. Hata wakati wa majaribu waona uzuri wa Mungu. Kuwaambia tu hivyo haitoshi. Bali waweze kuelewa hayo hata katika wakati mgumu. Pia wajue kwamba Mungu ni mwema.

 

Tukihubiri juu ya Mungu mkali watamwelewa Mungu kwa njia isiyo sahihi ndani ya mioyo yao. Tukihubiri juu ya Mungu wa upendo wao wanaona Mungu mwema. Hivyo tunapaswa mara nyingi kuhubiri juu ya upatanisho. Pia tuelekeze mawazo ya wasikilizaji juu ya dhabihu ya Golgotha. Huko Mungu anaonyesha upendo wake juu yetu ya wenye dhambi. Hubiri mara nyingi juu ya upatanisho na damu ya Yesu. Hivyo Wakristo wanajua Mungu ni mzuri na mwema.

 

Jambo la mwisho Daudi, mwandishi wa Zaburi anaa­ndika kwamba anafurahi kukaa ndani ya nyumba ya Mungu milele. Hiyo sio lazima bali hiari hivyo tuna­weza kumshukuru Mungu.

 

Marudio: Kwanza kondoo alifurahia malisho, maji ya utulivu kupumzika na uhuisho wa rohoni. Tena baada ya majaribu alifurahi kuweza kukaa ndani ya nyumba ya Mungu yaani kanisani. Sasa sio muhimu kwamba ana­pata nini katika wokovu bali kwamba anaweza kuabudu wapi au kukaa wapi.

 

Kondoo wanatofautiana sana. Ni sawa hata kanisani kuna Wakristo tofauti tofauti. Wao wanaona wokovu kwa njia tofauti. Mwingine anahui­shwa nafsi na mwingine anashtuka kuingia ndani ya bonde la giza. Wakati huo Mkristo anakula katika mali­sho mabichi na kunywa maji ya utulivu lakini mwingine ambaye alikuwa katika majaribu anafurahi anapopata kula ingawa ana majaribu.

 

Ni lazima mchungaji pia apate kula. Ni muhimu ili mchungaji pia apate chakula. Wakati mwingine mchu­ngaji anapata njaa wakati analisha kondoo. Au mchu­ngaji ana kiu ingawa anawanywesha wengine maji ma­safi ya baraka. Chakula cha mchungaji na kula kwake ni tofauti na kondoo. Wakristo wanapata chakula cha ki­roho na baraka za rohoni kanisani na mkutanoni.

 

Lakini wachungaji hawazipati mikutanoni kama watu wengine. Wachungaji sehemu yao ya chakula ni tofauti. Wao wanajitayarishia mara nyingi chakula chao. Yaani wa­chunguze zaidi ndani ya neno la Mungu. Wao wanata­kiwa wapate wenyewe chakula ndani ya mao­mbi. Haitosi tu wanapoenda mkutanoni.

 

Ni muhimu tukumbuke kwamba watu wote wanape­ndwa na Mchungaji Mkuu, Yesu Kristo. Nasi pia tuwa­pende. Kwa sababu alikuchagua ili aweze kufikisha kundi lake ndio maana alikuchagua uwe mchungaji. Kwa msaada wako anataka kuwa fikisha kundi lake nyumbani.

 

Biblia inasema: Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake;  (EFE 5:25b)

Upendo wake alionyesha Go­lgotha. Yeye anachunguza namna gani tunaenenda na kondoo wake. Tuulize: Unataka tulishe kondoo wako namna gani na kuwaongoza. Tunasubiri siku moja tu­weze kuliongoza kundi hili dogo mbele ya Mchungaji Mkuu. Na natumaini tunaweza kusema: Hakuna aliye baki, wote ni salama.

 

Nawasihi wazee walio kwenu, mimi niliye mzee, mw­enzi wao, na shahidi wa mateso ya Kristo, na mshirika wa utukufu utakaofunuliwa baadaye; lichugeni kundi la Mungu lililo kwenu, na kulisimamia, si kwa kulazimi­shwa, bali kwa hiari kama Mungu atakavyo; si kwa kutaka fedha ya aibu, bali kwa moyo. Wala si kama wajifanyao mabwana juu ya mitaa yao, bali kwa kujifa­nya vielelezo kwa lile kundi. Na Mchungaji mkuu ata­kapodhihirishwa, mtaipokea taji ya utukufu, ile isiyoka­uka. (1PET 5:1-4)

 

Mungu akubarikie sana na kazi yako!